Psalms 14:1-3

Uovu Wa Wanadamu

(Zaburi 53)

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 aMpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna hata mmoja atendaye mema.

2 b Bwana anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.
3 cWote wamepotoka,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!
Copyright information for SwhNEN